Hesperian Health Guides
Mshituko wa moyo
Katika sura hii:
- Huduma ya kwanza
- Weka utulivu na kudhibiti dharura
- Kupoteza fahamu (kuzirai)
- Kupumua
- Pasipo mapigo ya moyo
- Kutokwa damu
- Mshituko
- Vidonda
- Vidonda ambavyo vimeingia ndani
- Maambukizi
- Ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu (sepsisi)
- Tetanasi (pepopunda)
- Majeraha ya uti wa mgongo na shingo
- Majeraha ya kichwa
- Vidonda kwenye kifua na mbavu ambazo zimevunjika
- Majeraha na vidonda kwenye tumbo
- Mshituko wa moyo
- Mifupa iliyovunjika, kutenguka, na misuli au tishu zilizoumia
- Kuvia damu kutokana na majeraha chini ya ngozi
- Ubakaji
- Majeraha ya moto
- Kupigwa na umeme
- Kuunguzwa na kemikali
- Silaha za kipolisi
- Dharura zinazohusu afya ya akili
- Sumu
- Dharura zinazohusiana na ugonjwa wa kisukari
- Shambulio linalofanana la kifafa (seizures), mtukutiko wa maungo (convulsions)
- Kuumwa au kung'atwa na wadudu au viumbe wengine
- Mzio: Mzio mdogo au mzio mkali
- Dharura kutokana na joto kali
- Dharura kutokana na baridi kali
- Madawa
Wanawake na wanaume pia hupatwa na tatizo la mshituko wa moyo. Mshituko wa moyo hutokea pale mtiririko wa damu kwenye moyo unaposimama kwa muda mrefu na kusababisha sehemu ya moyo kuanza kufa. Kawaida hii husababishwa na ugonjwa wa moyo. Kwa taarifa zaidi juu ya ugonjwa wa moyo, angalia Magonjwa yasiopona (kinaandaliwa).
Dalili

- Kusikia shinikizo, kubanwa, kukabwa, hisia ya kuugua, na maumivu kifuani, au kifua kujaa
- Maumivu hayo yanaweza kuenea hadi shingoni, mabegani, mikononi, kwenye meno au taya
- Maumivu kawaida huja taratibu lakini wakati mwingine yanaweza kuwa ya ghafla na makali
- Pumzi nyepesi
- Kutokwa jasho
- Kichefuchefu
Maumivu kifuani ndiyo dalili kuu ya kawaida kwa ajili ya wanawake na wanaume, lakini wanawake mara nyingi hawahisi maumivu kifuani. Badala yake huhisi pumzi nyepesi, uchovu, kichefuchefu, kutapika, au maumivu mgongoni au kwenye taya.
Matibabu
Mpe kidonge 1 cha aspirini mara moja. Mwambie akitafune na kumeza na maji. Hata kama huna uhakika kwamba mtu anapata mshituko wa moyo, aspirini haitampa madhara.
Kama unayo, mpe dawa ya naitroglaserini (nitroglycerine) ambayo huwekwa chini ya ulimi ili iweze kuyeyuka na kufyonzwa na mwili. Mofini (morphine) pia husaidia kupunguza maumivu na woga. Mpe matumaini mgonjwa na tafuta msaada.