Hesperian Health Guides
Kuunguzwa na kemikali
Katika sura hii:
- Huduma ya kwanza
- Weka utulivu na kudhibiti dharura
- Kupoteza fahamu (kuzirai)
- Kupumua
- Pasipo mapigo ya moyo
- Kutokwa damu
- Mshituko
- Vidonda
- Vidonda ambavyo vimeingia ndani
- Maambukizi
- Ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu (sepsisi)
- Tetanasi (pepopunda)
- Majeraha ya uti wa mgongo na shingo
- Majeraha ya kichwa
- Vidonda kwenye kifua na mbavu ambazo zimevunjika
- Majeraha na vidonda kwenye tumbo
- Mshituko wa moyo
- Mifupa iliyovunjika, kutenguka, na misuli au tishu zilizoumia
- Kuvia damu kutokana na majeraha chini ya ngozi
- Ubakaji
- Majeraha ya moto
- Kupigwa na umeme
- Kuunguzwa na kemikali
- Silaha za kipolisi
- Dharura zinazohusu afya ya akili
- Sumu
- Dharura zinazohusiana na ugonjwa wa kisukari
- Shambulio linalofanana la kifafa (seizures), mtukutiko wa maungo (convulsions)
- Kuumwa au kung'atwa na wadudu au viumbe wengine
- Mzio: Mzio mdogo au mzio mkali
- Dharura kutokana na joto kali
- Dharura kutokana na baridi kali
- Madawa

Jikinge kwanza: Vaa vazi lenye mikono mirefu na glovu juu ya mikono yako. Funika mdomo wako na kitambaa. Nawa vizuri na kufua nguo zako kikamilifu baada ya kumsaidia mtu yeyote ambaye amechafuliwa au kufikiwa na kemikali.
Njia bora zaidi ya kuzuia madhara kutokana na kuunguzwa na kemikali ni kuondoa kemikali husika haraka iwezekanavyo.
- Ondoa nguo na vito karibu na jeraha.
- Kama kemikali inanata, haraka kwangua kwa kutumia kijiti au kitu chochote imara ambacho ni bapa.
- Mara baada ya kuondoa kemikali yote ambayo unaweza, suuza eneo hilo na maji mengi sana. Maji yanaweza kusababisha baadhi ya kemikali kuanza kuungua. Hivyo hakikisha kuwa unaondoa kiasi kikubwa cha kemikali kadri uwezavyo. Kwa kemikali yenye mafuta, tumia sabuni na maji. Tumia mpira au bomba. Kama uso umedhurika, osha vizuri kwanza. Hasa safisha michaniko au sehemu zote za uwazi kwenye ngozi. Kadri utakavyowahi kunawa na kutumia muda mfupi kunawa ndivyo utakuwa katika nafasi bora zaidi kunusuru ngozi yako.
Baada ya kuosha kemikali yote kutoka kwenye mwili wa mtu aliyedhurika, tibu sehemu iliyounguzwa na kemikali kama jinsi unavyotibu
vidonda vingine vya moto.
Osha au tupa nguo zozote ambazo zimeguswa na kemikali, kwani zinaweza kusababisha madhara.
![]() |
Kama kemikali zitaingia machoni, tiririsha maji kwenye jicho ukianzia ndani ya jicho (karibu na pua) kuelekea nje ya jicho (karibu na sikio). |