Hesperian Health Guides
Kuvia damu kutokana na majeraha chini ya ngozi
HealthWiki > Toleo Jipya: Mahali Pasipo na Daktari > Huduma ya kwanza > Kuvia damu kutokana na majeraha chini ya ngozi
Katika sura hii:
- Huduma ya kwanza
- Weka utulivu na kudhibiti dharura
- Kupoteza fahamu (kuzirai)
- Kupumua
- Pasipo mapigo ya moyo
- Kutokwa damu
- Mshituko
- Vidonda
- Vidonda ambavyo vimeingia ndani
- Maambukizi
- Ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu (sepsisi)
- Tetanasi (pepopunda)
- Majeraha ya uti wa mgongo na shingo
- Majeraha ya kichwa
- Vidonda kwenye kifua na mbavu ambazo zimevunjika
- Majeraha na vidonda kwenye tumbo
- Mshituko wa moyo
- Mifupa iliyovunjika, kutenguka, na misuli au tishu zilizoumia
- Kuvia damu kutokana na majeraha chini ya ngozi
- Ubakaji
- Majeraha ya moto
- Kupigwa na umeme
- Kuunguzwa na kemikali
- Silaha za kipolisi
- Dharura zinazohusu afya ya akili
- Sumu
- Dharura zinazohusiana na ugonjwa wa kisukari
- Shambulio linalofanana la kifafa (seizures), mtukutiko wa maungo (convulsions)
- Kuumwa au kung'atwa na wadudu au viumbe wengine
- Mzio: Mzio mdogo au mzio mkali
- Dharura kutokana na joto kali
- Dharura kutokana na baridi kali
- Madawa
Kuvia damu humaanisha kuwa tishu chini ya ngozi imejeruhiwa na damu inavuja kutoka kwenye mishipa ya damu. Kuvia damu kunaweza kuwa na maumivu makali na kusababisha kero kwa majeruhi, lakini kawaida sio tatizo kubwa. Tibu tatizo la kuvia damu kama jinsi inavyotakiwa kutibu tatizo la majeraha ya tishu au kiungo chini ya ngozi (kutokana na kujisokota au au kuchanika): tibu kwa kupumzika vya kutosha, barafu, mgandamizo, na kuinua sehemu iliyojeruhiwa.
Kuvia damu kichwani au tumboni inaweza kuwa dalili ya tatizo kubwa zaidi. Angalia jinsi ya kufanya kama siku za karibuni mtu huyu alipata kipigo kikali kichwani au tumbo.
Kama utaona mtu anavilia damu mara kwa mara, au ana majeraha ya aina hiyo katika hatua tofauti za uponaji, hii inaweza kuwa dalili kuwa anafanyiwa mateso na ukatili. Angalia Vurugu (kinaandaliwa).