Hesperian Health Guides
Ubakaji
Katika sura hii:
- Huduma ya kwanza
- Weka utulivu na kudhibiti dharura
- Kupoteza fahamu (kuzirai)
- Kupumua
- Pasipo mapigo ya moyo
- Kutokwa damu
- Mshituko
- Vidonda
- Vidonda ambavyo vimeingia ndani
- Maambukizi
- Ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu (sepsisi)
- Tetanasi (pepopunda)
- Majeraha ya uti wa mgongo na shingo
- Majeraha ya kichwa
- Vidonda kwenye kifua na mbavu ambazo zimevunjika
- Majeraha na vidonda kwenye tumbo
- Mshituko wa moyo
- Mifupa iliyovunjika, kutenguka, na misuli au tishu zilizoumia
- Kuvia damu kutokana na majeraha chini ya ngozi
- Ubakaji
- Majeraha ya moto
- Kupigwa na umeme
- Kuunguzwa na kemikali
- Silaha za kipolisi
- Dharura zinazohusu afya ya akili
- Sumu
- Dharura zinazohusiana na ugonjwa wa kisukari
- Shambulio linalofanana la kifafa (seizures), mtukutiko wa maungo (convulsions)
- Kuumwa au kung'atwa na wadudu au viumbe wengine
- Mzio: Mzio mdogo au mzio mkali
- Dharura kutokana na joto kali
- Dharura kutokana na baridi kali
- Madawa
Ngono ya kulazimisha, ngono ambayo haihitajiki au siyo ya kuridhia, ni ubakaji. Wanawake na wasichana wanaweza kubakwa na watu wanaowafamu, wapita njia, wanafamilia, au waume zao au marafiki wa kiume. Wanaume na wavulana nao wanaweza kubakwa. Kwa taarifa zaidi juu ya ubakaji, angalia sura juu ya Vurugu (inaandaliwa).
Mtu ambaye amebakwa atahitaji huduma ya kwanza kwa ajili ya majeraha ya kimwili. Pia atahitaji msaada wa kisaikilojia na huduma mbalimbali. Mhudumie kwa huruma na uelewa wa hali yake. Usimlaumu.

Ubakaji unaweza kusababisha mimba. Dozi kubwa ya vidonge vya majira inaweza kuzuia mimba. Angalia Uzazi wa mpango. Ubakaji pia unaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa ya ngono. Angalia Maambukizi sehemu za ukeni au umeni na matatizo mengine (kinaandaliwa). Ili kuzuia maambukizi ya VVU baada ya ubakaji, angalia VVU na UKIMWI (kinaandaliwa).
Inaweza kuwa vigumu kwa mtu aliyebakwa kukurusu kumuangalia au kumgusa. Elezea utakachofanya katika kumchunguza na kutoa matibabu na omba ruksa yake kabla ya kumgusa.
Kama via vyake vya uzazi vina michaniko au michubuko, vinaweza kutoa maumivu. Mpe asetaminofeni au ibuprofeni. Kama kuna damu nyingi inatoka kwenye njia ya haja kubwa au ukeni, tumia mgandamizo kusimamisha uvujaji damu. Mfundishe jinsi ya kuizuia mwenyewe, kama damu itaendelea kutoka tena baadaye.
Kwa ajili ya mikwaruzo na michubuko midogo, loweka via vya uzazi kwenye maji ya vuguvugu mara 3 kila siku. Kumwaga maji juu ya via vya uzazi wakati wa kukojoa husaidia kupunguza hisia za mwako au kuungua. Michaniko mikubwa inaweza kuhitaji kushonwa.

Chunguza iwapo kuna majeraha sehemu zingine za mwili pia. Angalia sehemu zingine za sura hii jinsi ya kutibu matatizo mahsusi. Kutunza kumbukumbu au taarifa za uchunguzi wa kimwili na majeraha ni muhimu kama mwanamke atatoa taarifa juu ya tukio polisi—hata kama atakwenda kutoa taarifa baadaye sana.
Mfuatilie mwanamke huyu baada ya siku chache kujua anaendeleaje kisaikolojia na kimwili. Chunguza michaniko na michubuko kwa ajili ya dalili za maambukizi. Maambukizi ya kibofu (angalia Matatizo katika kukojoa — kinaandaliwa) hujitokeza sana baada ya ngono ya kulazimisha au isiyoridhiwa.