Hesperian Health Guides
Ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu (sepsisi)
HealthWiki > Toleo Jipya: Mahali Pasipo na Daktari > Huduma ya kwanza > Ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu
Katika sura hii:
- Huduma ya kwanza
- Weka utulivu na kudhibiti dharura
- Kupoteza fahamu (kuzirai)
- Kupumua
- Pasipo mapigo ya moyo
- Kutokwa damu
- Mshituko
- Vidonda
- Vidonda ambavyo vimeingia ndani
- Maambukizi
- Ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu (sepsisi)
- Tetanasi (pepopunda)
- Majeraha ya uti wa mgongo na shingo
- Majeraha ya kichwa
- Vidonda kwenye kifua na mbavu ambazo zimevunjika
- Majeraha na vidonda kwenye tumbo
- Mshituko wa moyo
- Mifupa iliyovunjika, kutenguka, na misuli au tishu zilizoumia
- Kuvia damu kutokana na majeraha chini ya ngozi
- Ubakaji
- Majeraha ya moto
- Kupigwa na umeme
- Kuunguzwa na kemikali
- Silaha za kipolisi
- Dharura zinazohusu afya ya akili
- Sumu
- Dharura zinazohusiana na ugonjwa wa kisukari
- Shambulio linalofanana la kifafa (seizures), mtukutiko wa maungo (convulsions)
- Kuumwa au kung'atwa na wadudu au viumbe wengine
- Mzio: Mzio mdogo au mzio mkali
- Dharura kutokana na joto kali
- Dharura kutokana na baridi kali
- Madawa
Hali hii hutokea pale maambukizi yanapoenea hadi kwenye mfumo wa damu. Ni hali ya hatari kwa sababu huweza kusababisha mshituko. Kama unafikiri sumu ya ambukizo imeanza kuenea kwenye damu, tafuta msaada wa kitabibu haraka na mgonjwa atibiwe wakati mkiwa njiani.

Dalili za ueneaji wa sumu ya vimelea kwenye damu (sepsisi)
- Homa au kiwango cha joto la mwili kinashuka chini sana
- Mapigo ya moyo yanakwenda haraka — mapigo ya moyo zaidi ya 90 kwa dakika.
- Kupumua haraka — zaidi ya pumzi 20 kwa dakika
- Kupumua kwa shida
- Ngozi ya mwili kupauka au kuweka alama
- Kutoa mkojo kidogo
- Kuchanganyikiwa au kupoteza ufahamu
- Shinikizo la damu kwenda chini ya kiwango kinachohitajika
Dalili muhimu zaidi ni homa au kushuka sana kwa kiwango cha joto la mwili, mapigo ya haraka ya moyo, na kupumua haraka. Kama mtu ana dalili kama hizi 2 au zaidi, mpe tiba dhidi ya ueneaji wa sumu kwenye damu (sepsisi).
Matibabu
Tafuta msaada wa kitabibu. Ukiwa njiani:
- Angalia iwapo kuna dalili zozote za mshituko na kutoa matibabu.
- Mpe seftriaksoni (ceftriaxone), AU sipro (ciprofloxacin) pamoja na klindamaisini (clindamycin).
- Safisha vidonda vyote ambavyo vimepata maambukizi, ondoa ngozi iliyokufa, na kamua majipu na vimbe ili kutoa usaha. Kujifunza zaidi juu ya kukamua jipu, angalia Matatizo ya ngozi, kucha, na nywele (inaandaliwa).
- Kama mgonjwa anapumua vizuri, mpe vinywaji. Mpe kidogo baada ya kila muda mfupi.