Hesperian Health Guides

Vidonda kwenye kifua na mbavu ambazo zimevunjika

Katika sura hii:

Dereva akiwa kwenye gari ambayo imepata ajali.
Kuanguka au kugongana na kitu kigumu kwa nguvu kunaweza kusababisha mbavu nyingi kuvunjika kwa mpigo.

Maumivu yanayochoma pale mtu ambaye amejeruhiwa kifuani anapopumua au kukohoa, au kuhisi ulaini sehemu inapoguswa, vinaweza kuashiria mbavu zilizovunjika. Chunguza mbavu na kuzigusa na vidole vyako. Kama kuna sehemu ambayo imejitokeza juu chini ya ngozi, au mahali ambapo ikibonyezwa inaingia ndani na ni laini sana, mbavu hiyo imevunjika. Kama ni mbavu moja ambayo imevunjika na haijajitokeza chini ya ngozi au nje ya mwili, mpe dawa ya kupunguza maumivu. Anapaswa kuepuka kubeba vitu na kazi nzito kwa wiki kadhaa. Itapona bila matibabu maalum. Mkumbushe kupumua pumzi nzito kila baada ya saa chache. Hii inaumiza lakini husaida kuwezesha mapafu kuendelea kufanya kazi.

Mbavu nyingi kuvunjika

  1. Tumia kitambaa kilichokunjwa au pedi nzito iliyokunjwa na plasta kufunika mbavu zilizovunjika.

  2. NWTND fa Page 25-1.png


  3. Mlaze majeruhi katika hali yoyote ile inayomsaidia kupumua.
  4. Chunguza iwapo kuna dalili za mshituko na kutafuta msaada.

Vidonda kwenye kifua ambavyo vimeingia ndani

Kupigwa risasi, kuchomwa na kitu kikali, mlipuko, au mbavu ambayo imevunjika vibaya sana inaweza kusababisha hewa kuingia ndani na nje ya mapafu.

  1. Bila kuchelewa, funika uwazi huo ili hewa isingie kwa kutumia mathalan, bandeji ambayo imepakwa mafuta ya jeli, mfuko wa nailoni uliokunjwa vizuri, au hata jani la mgomba.
  2. Funga na plasta pande 3 tu ili hewa iweze kutoka lakini siyo kuingia.
  3. Bandeji ya pembe nne ikiwa imefungwa juu kwa kutumia plasta, upande wa juu na pembeni ya kifua cha majeruhi.
  4. Mlaze katika nafasi yoyote ile itakayomwezesha kupumua. Tafuta msaada.