Hesperian Health Guides
Sura ya 15: Utoaji mimba na matatizo yanayotokana na utoaji mimba
HealthWiki > Pale ambapo Wanawake hawana Daktari > Sura ya 15: Utoaji mimba na matatizo yanayotokana na utoaji mimba
Kama njia za uzazi wa mpango zitashindikana, angalau utoaji mimba kisheria ni njia salama kiasi kwa mwanamke |
Ukosefu wa huduma za uzazi wa mpango na ukosefu wa taarifa sahihi juu ya ngono huchangia mimba zisizotakiwa na utoaji mimba.
Mwanamke anapofanya kitendo chochote kukatisha ujauzito ni utoaji mimba. Katika kitabu hiki, neno utoaji mimba linaelezea tu kitendo cha makusudi ambacho kimepangwa. Tukio la ujauzito kutoka au kukatishwa kwa bahati mbaya hujulikana kama mimba kuharibika (miscarriage).