Hesperian Health Guides
Dawa za vidonda kutokana na kuungua
HealthWiki > Toleo Jipya: Mahali Pasipo na Daktari > Huduma ya kwanza > Dawa za vidonda kutokana na kuungua
Majeraha ya kuungua yanaweza kupata maambukizi. Hivyo toa antibiotiki kama vile dikloksasilini (dicloxacillin), kilindamaisini (clindamycin), sefaleksini (cephalexin), AU sipro (ciprofloxacin) kama kuna dalili ya maambukizi.
Kadri kidonda kinavyoendelea kupona, mpe dawa kutoka kundi la antihistamini kama vile klorofeniramini (chlorpheniramine) AU difenhidramini (diphenhydramine) kupunguza mwasho.
Mpe chanjo ya tetanasi kama ratiba yake ya chanjo za tetanasi siyo kamilifu (angalia Chanjo – inaandaliwa).
Kama mtu alikuwa kwenye moto na kumeza moshi mwingi, dawa ya salbutamo (salbutamol) inaweza kumsaidia aweze kupumua vizuri.