Hesperian Health Guides

Wafanyakazi wa afya wanaweza kutoa msaada zaidi kwa watu wenye saratani

HealthWiki > Toleo Jipya: Mahali Pasipo na Daktari > Wafanyakazi wa afya wanaweza kutoa msaada zaidi kwa watu wenye saratani

Katika sura hii:

Wafanyakazi wa afya wa jamii wanaweza kujifunza juu ya uzuiaji na matibabu ya saratani na kuwasaidia wanajamii wengine pia kujifunza.

Msaidie mtu mwenye saratani na familia:

  • Kutojisikia wapweke.
  • Watambulishe kwa watu wengine ambao nao wamepitia uzoefu unaofanana.
  • Wasaidie katika kutafuta vyakula vyenye afya, usafiri, na hata usimamizi wa nyumba na watoto wao, ikiwezekana kwa kushirikisha wanandugu, vikundi vya kijamii, makanisa au misikiti, na huduma za serikali.
  • Tunza orodha ya kliniki, madaktari, na taasisi ambazo husaidia watu wenye saratani katika eneo, wilaya, mkoa au nchi yako.
  • Msaidie mtu mwenye saratani kudhibiti maumivu, kero au kutojisikia vizuri, na wasiwasi au uoga.
  • Wasaidie watu wenye saratani na familia zao kuepuka watu wadanganyifu ambao watachukua fedha zao na kuahidi uponyaji wa kimiujiza ambao haupo au utafanya hali zao kuwa mbaya zaidi.
mfanyakazi wa afya akiongea na mwanamke.n.

Changia juhudi za kuongeza uelewa na uzuiaji wa saratani:

  • Himiza watu kujifunza dalili za mwanzo za saratani na kutoogopa kwenda kupimwa kwa sababu kupima mapema ni muhimu sana.
  • Saidia kufundisha makundi kuacha uvutaji wa tumbaku na madawa ya kulevya.
  • Elimisha jamii juu ya umuhimu wa chanjo dhidi ya homa ya manjano (hepatitis B) na kirusi cha HPV.
  • Himiza wanawake kuchuguzwa saratani ya shingo ya kizazi na saratani zingine kama huduma ya uchunguzi wa saratani inatolewa katika eneo lako.
  • Tafuta fursa za mafunzo kwa ajili yako na wafanyakazi wengine kuweza kutibu baadhi ya saratani. Wakunga wanaweza kujifunza kuchunguza na kuzuia baadhi ya saratani.
  • Wasaidie watu kujipanga kuzuia kemikali zenye sumu na vichafuzi vingine kuingia kwenye vyanzo vya maji ya jamii, ardhi na hewa.
  • Himiza jamii kuwasaidia na kuwatendea watu wenye saratani kwa huruma, na siyo kuwalaumu kwa ajili ya magonjwa yao.