Hesperian Health Guides
Dawa zingine za kutibu kuhara
HealthWiki > Toleo Jipya: Mahali Pasipo na Daktari > Maumivu tumboni, kuhara, na minyoo > Dawa zingine za kutibu kuhara
Furoti Diloksanaidi (Diloxanide furoate)
Diloksanaidi (Diloxanide) hutumika pamoja na antibiotiki kutibu ameba. Kama huwezi kupata dawa hii, jaribu paromomaisini (paromomycin) au iodokino (iodoquinol) badala yake.
![Green-effects-nwtnd.png](https://pool.hesperian.org/w/images/thumb/4/42/Green-effects-nwtnd.png/25px-Green-effects-nwtnd.png)
Kwa nadra dawa hii husababisha gesi tumboni, maumivu tumboni, au kichefuchefu. Tumia na chakula.
![NBgrnimportant.png](https://pool.hesperian.org/w/images/thumb/0/08/NBgrnimportant.png/30px-NBgrnimportant.png)
Usitumie diloksanaidi (diloxanide) ndani ya miezi 3 ya kwanza ya ujauzito. Epuka dawa hii wakati unapokuwa unanyonyesha.
![NBgrnpill.png](https://pool.hesperian.org/w/images/thumb/1/17/NBgrnpill.png/25px-NBgrnpill.png)
Baada ya kumaliza dozi ya metronidazo au tiba nyingine ya ameba, anza kutumia diklosanaidi (diloxanide).
Chini ya miaka 3: toa miligramu 62 (⅛ ya kidonge cha miligramu 500), mara 3 kila siku kwa siku 10.
Miaka 3 hadi 7: toa miligramu 125, mara 3 kila siku kwa siku 10.
Miaka 8 hadi 12: toa miligramu 250, mara 3 kila siku kwa siku 10.
Zaidi ya miaka 12: toa miligramu 500, mara 3 kila siku kwa siku 10.
Kwinakrini (Quinacrine)
Dawa ya Kwinakrini (Quinacrine) hufanya kazi vizuri katika kutibu giardia, lakini huwafanya watu kujisikia vibaya zaidi. Hutumika kwa sababu siyo ghali sana.
![Green-effects-nwtnd.png](https://pool.hesperian.org/w/images/thumb/4/42/Green-effects-nwtnd.png/25px-Green-effects-nwtnd.png)
Maumivu ya kichwa, kizunguzungu, na kutapika ni madhara ya kawaida.
![NBgrnpill.png](https://pool.hesperian.org/w/images/thumb/1/17/NBgrnpill.png/25px-NBgrnpill.png)
Zaidi ya miaka 10: toa miligramu 100, mara 3 kila siku kwa wiki 1.
Zinki
Zinki husaidia watu wanaoharisha kupata nafuu haraka. Inapaswa kutolewa pamoja na kinywaji cha kuuongezea mwili maji.
![NBgrnpill.png](https://pool.hesperian.org/w/images/thumb/1/17/NBgrnpill.png/25px-NBgrnpill.png)
Kwa watoto wachanga, vidonge vinaweza kusagwa na kuchanganywa na maziwa ya mama au maji kidogo. Unaweza kupata kidonge ambacho huyeyuka haraka kwenye maji au kimiminika kingine.
Zaidi ya miezi 6: toa miligramu 20, mara moja kila siku kwa siku 10 hadi 14.