Hesperian Health Guides

Upandaji miti

Katika sura hii:

Katika hali nzuri ya kawaida, upandaji miti husaidia ardhi iliyoharibiwa kurejeshewa uhai wake na kutoa kuni, mbao, chakula kwa binadamu na wanyama, pamoja na dawa. Upandaji miti unaweza kuifanya ardhi iliyochakaa na isiyozalisha kuwa na rutuba na kuzalisha tena. Hata hivyo, miti iliyopandwa katika hali ngumu, inahitaji matunzo ili iweze kukua vizuri. Upandaji miti una faida nyingi, lakini haufai kwa maeneo yote au jamii zote. Soma “Tumia maarifa ya kila mtu, zingatia mahitaji ya kila mtu”.

A tall tree next to 2 seedlings.

Zipo njia mbalimbali za kupanda miti:


Njia utakayoichagua itategemea na aina ya miti unayotaka kupanda, na mbegu au vipandikizi vilivyopo.

Kuchagua mbegu au vipandikizi

Watu wengi wanaamini msemo kuwa “Kama alivyo mzazi na mtoto wake ndivyo atakavyokuwa”. Hivyo, mtoto ambaye wazazi wake ni warefu, naye hutarajiwa kuwa mrefu. Hivi ndivyo ilivyo hata kwa mimea. Mbegu kutoka mti mrefu ulionyooka huenda ikazaa mti ambao unafaa kwa ajili ya mbao. Mbegu kutoka kwenye mti wenye sifa za dawa pia hutarajiwa kuzaa mti wenye sifa hizo hizo. Hivyo, ni bora kuchagua mbegu au vipandikizi kutoka mti-mama wenye afya na sifa unazotaka. Iwapo huwezi kupata mbegu bora katika eneo lako, unaweza kupata mbegu hizo kutoka kwa wakala wa ugani, au vitalumiche katika maeneo ya jirani.

Maandalizi ya mbegu kwa ajili ya kupanda

Baadhi ya mbegu, hususan zile zenye ganda laini, unga au majimaji ndani yake, lazima zipandwe mara baada ya kukusanywa. Mbegu nyingine huhitaji kuhifadhiwa kwa miezi mingi kabla ya kupandwa.

EHB Ch11 Page 207-1.png

Mbegu nyingi zinahitaji maji ili ziweze kuota. Mbegu inapokuwa imefunikwa na ganda gumu inaweza pia kuhitaji kulainishwa au kukatwa kuruhusu ufyonzaji wa maji. Baadhi ya mbegu zinahitaji maandalizi zaidi kabla ya kupandwa.

  • Kama ganda la mbegu siyo gumu sana (iwapo unaweza kuitoboa na kucha zako za vidole) na siyo nene sana, basi panda moja kwa moja kwenye udongo uliolowa.
EHB Ch11 Page 207-2.png
  • Kama ganda ni gumu lakini jembamba, funga mbegu ndani ya kitambaa. Ziloweshe kwa muda wa dakika 1 kwenye maji yasiyo ya moto sana, ambayo unaweza kugusa na vidole vyako (hayajafikia kuchemka). Zitoe haraka kwenye maji ya moto na kuziweka kwenye maji baridi na zibaki humo usiku mzima. Zipandwe siku inayofuata.
  • Njia nyingine ya kushughulikia mbegu zenye ganda gumu lakini jembamba ni kuziloweka kwenye maji baridi kwa muda wa siku nzima. Baada ya hapo, zifunge kwenye tambaa au gunia ambalo limelowesha na maji kwa muda wa saa nyingine 24. Rudia utaratibu huu kwa muda wa siku 6. Siku ya saba zipande.
EHB Ch11 Page 207-3.png
  • Kama ganda ni gumu na nene, sugua mbegu kwa kutumia kipande cha karatasi - mchanga (sand paper) au chochote kinachofaa hadi sehemu laini za ndani ya mbegu zionekane. Chukua tahadhari usisugue sana sehemu za ndani na kuharibu mbegu.

EHB Ch11 Page 207-4.png

  • Baadhi ya mbegu zenye ganda gumu huandaliwa kwa kulowekwa kwenye maji usiku mzima zikiwa zimechanganywa na samadi, halafu huanikwa juani kwa siku moja. Rudia utaratibu huu kwa siku 3 - 4. Mbegu nzuri zitachipua tayari kwa ajili ya kupandwa. Mbegu ambazo hazitachipua zisitumike.


Baadhi ya mbegu huhitaji maandalizi ya kina zaidi, kama vile kupashwa katika moto mdogo, kuwekwa kwenye ubaridi mkali, au kwanza kuliwa na wanyama na kutolewa kama sehemu ya kinyesi. Fanya majaribio kujua njia ipi inafaa. Baada ya majaribio kadhaa, unaweza kuwa mtaalamu wa kuanzisha vitalu-miche.

Kuandaa vipandikizi - miche

EHB Ch11 Page 208-1.png
Panda kwa usawa wa pembe hii.
Fundo 3 hadi 4 ziwe ndani ya udongo
Mizizi huota kutoka kwenye fundo ndani ya udongo.

Baadhi ya miti huota vizuri kwa kupanda vipandikizi - miche ardhini na kuvimwagilia maji hadi kuanza kutoa mizizi na majani. Miti inayoota kutokana na vipandikizi - miche, kwa kawaida hutoa matunda au mbegu mapema zaidi kuliko ile inayooteshwa kwa kutumia mbegu. Baadhi ya vipandikizi-miche vinaweza kupandwa moja kwa moja ardhini sehemu unapotaka mti uote. Vingine huoteshwa kwenye kitalu mpaka vitakapochipua na kutoa majani na mizizi mingi na hivyo kuweza kuendelea kukua vyenyewe.

Kata vipande vya mti kutoka katikati ya tawi ambalo haliwezi kupinda sana wala kushindwa kupinda kabisa. Chagua kipande chenye fundo 6-10 (uvimbe kwenye tawi la mti mahali majani huota). Taratibu ondoa majani kwa uangalifu ili usiharibu fundo hizo. Kata tawi kwa pembe ya kuchonga na siyo pembe ya nyuzi 90 ili kuwezesha mizizi kuota vizuri.

Vipandikizi-miche, viwe vimepandwa kwenye kitalu-miche au moja kwa moja ardhini, vinapaswa kumwagiliwa maji mengi na kulindwa dhidi ya wadudu wasumbufu hadi vitakapokuwa vimeota mizizi ya kutosha kuweza kujitafutia maji vyenyewe.

A woman kneels to dig up a seedling

Kupandikiza miche-pori

Njia nyingine ya kuanzisha msitu ni kuchimbua miche ya miti ya porini na kuipandikiza pale unapotaka iote. Tafuta miti -mama iliyostawi vizuri na chagua miche mizuri inayoota karibu na miti hiyo.

Chimbua miche midogo kwa uangalifu ili usiharibu mzizi mkuu. Iwapo mzizi mkuu utaharibiwa, mti hautakua vizuri. Chimba kwa kufuata mduara kuzunguka mche na nenda chini mpaka utakapofikia ule mzizi mkubwa ulikoishia. Tumia mkono au kifaa kingine kung’oa mche na bila kuondoa udongo unaozunguka mizizi.

Acha udongo huo kwenye mizizi ya mche hadi utakapopandwa kwenye udongo. Endelea kumwagilia maji hadi mizizi itakapoweza kujitafutia maji yenyewe.

Kuotesha miti kwenye vitalu-miti

Vitalu-miti huwezesha miche kuanza kuota vizuri kabla ya kuhamishiwa kwenye maeneo mengine. Lakini kuanzisha na kutunza kitalu-miti siyo kazi rahisi. Inaleta maana kuanzisha kitalu - miti pale tu:

  • Mbegu au miche ambavyo unataka kupanda ni adimu.
  • Wadudu wasumbufu wanaweza kuharibu miche kama haikutunzwa vizuri.
  • Watu wana muda wa kutosha kuhudumia kitalu-miti.


Kupanda miti moja kwa moja ni rahisi zaidi kuliko kuipanda kwenye kitalu-miti kwanza na kuihamisha baadae. Hata hivyo, miche zaidi hufa inapopandwa moja kwa moja kuliko inapooteshwa kwenye vitalu.

Lini uanze kupanda miti?

Kipindi gani cha mwaka ambapo miti inapaswa kupandwa hutegemea muda ambao miche inastahili kubaki kwenye kitalu-miche. Kama eneo lako lina msimu wa masika na kiangazi, panda miti yako pale tu masika yanapoanza ili kuepuka kazi ya kumwagilia. Miti mingi inahitaji miezi 3-4 kuwa kwenye kitalu kabla haijakuwa tayari kupandwa sehemu nyingine.

Mahali pa kuweka kitalu-miche

Kitalu -miche kinapaswa kufikika kwa urahisi, na ku wepo muda wote ambao miche inahitaji kukua kabla haijahamishwa na kupandwa sehemu nyingine. Pia kitalu-miche kiweze kufikiwa kwa urahisi na wote wanaokihudumia.

Kila kitalu-miche kinahitaji mambo yafuatayo:

Sw EHB Ch11 Page 209-1.png
Chanzo cha maji na mfumo wa kuhifadhi maji
Sehemu salama kwa ajili ya kutunzia vifaa
Sehemu kwa ajili ya kuchanganyia udongo na kujazia vifaa

Kinga dhidi ya jua, mvua na upepo kupita kiasi
Wigo kuzuia wanyama wakubwa na waharibifu wengine
Nafasi kwa ajili ya miche yote
Eneo tambarare au lenye tungazi kama kwenye mteremko wa milima

Kuotesha miche ya miti kwenye vyombo

Kuotesha miche ya miti kwenye vyombo hurahisisha kuisafirisha na kupanda. Vyombo vinatakiwa kuwa vipana na vyenye kina cha kutosha kuwezesha miche kukua na kujega tuta la udongo kwenye mizizi, lisilo kubwa sana kiasi cha kuzidi uzito, au kufyonza maji zaidi kuliko mahitaji ya mche.

Urefu wa muda ambao mche unahitaji kubaki kwenye kitalu-miti, ndivyo ukubwa wa chombo kinachotakiwa. Ukubwa mzuri wa miti mingi kawaida ni angalau inchi 6 upana na inchi 9 kwenda chini. Vyombo vinapaswa kuwa imara kuweza kusimama wima vitakapojazwa udongo, na viwe na matundu kutoa nje maji pale yanapozidi.

Seedlings in different types of containers.
Vyombo ambavyo vimetengenezwa kutokana na malighafi ambayo inaweza kuoza, mathalan magazeti, majani, karatasi ngumu, vinaweza kuchimbiwa moja kwa moja kwenye udongo pamoja na mche uliopo kwenye chombo. Vyombo ambavyo vimetengenezwa kwa plastiki, udongo wa mfinyanzi, mchanganyiko wa mchanga na saruji, bilauri au mbao vinapaswa kuondolewa kabla ya kupanda, lakini vinaweza kutumika tena mara kadhaa.Miche michanga inahitaji kulindwa dhidi ya jua kali.
Miche michanga inahitaji kulindwa dhidi ya jua kali. Kawaida miti mingi huota vizuri zaidi chini ya kivuli, hasa wakati wa jua kali la mchana.

Udongo wa kupandia

Udongo mahali miche inapopandwa unapaswa kuwa laini ili mizizi ya miche isioze. Pia, unapaswa kuwa na rutuba ili miche iweze kukua vizuri. Udongo kutoka kwenye msitu au kwenye kingo za mito au vijito ni mzuri kwa ajili ya miche.


Jinsi ya kupanda mbegu au vipandikizi-miti kwenye vyombo

  1. Mwagilia maji udongo vizuri siku kabla ya kupanda ili uwe laini lakini usilowe sana. Andaa mbegu kabla ya kupanda, lakini siyo muda mrefu kabla ya kupandwa ili zisianze kuota au kuoza.
  2. A watering can sprinkles a container.

  3. Katika kupanda mbegu ndogo sana, kwaruza udongo wa juu, rashia mbegu 5 au 10, na kufukia kidogo kwa taka nyepesi, ukikwaruza tena na reki au kijiti.
    Katika kupanda mbegu kubwa, chimba shimo mara 2-3 ukubwa wa mbegu. Unaweza kupanda zaidi ya mbegu moja kwenye kila chombo. Funika mbegu kwa taka na shindilia polepole. Kushindilia taka pole pole husaidia kuondoa hewa yoyote ndani ambayo inaweza kutoa nafasi kwa ukungu kuota.
  4. Mwagilia maji kwenye vyombo baada ya kupanda. Kama mbegu ni ndogo sana, mwagilia maji kwa uangalifu ili zisipotee.
  5. Mbegu zitakapochipua na kutoa jani 1 au 2, chagua mche ambao unaonekana umestawi vizuri na kata miche mingine yote, ukiacha mche mmoja mmoja katika kila chombo. Kwa kukata hiyo miche mingine kuliko kuing’oa, hutaathiri mizizi ya mche ambao unataka ubaki.


Kumwagilia miche ya miti

Illustration of the below: A drooping seedling next to an upright seedling.
Mti huu unahitaji maji
Mti huu una maji ya kutosha

Umwagiliaji wa miche ni moja ya kazi muhimu katika kitalu. Unapaswa kumwagilia miti yako kwa kunyeshea taratibu kama mvua, badala ya kuachia maji kwenye mtiririko mmoja kama bomba, hali ambayo inaweza kuondoa udongo na kufukua mizizi.

Kiasi cha maji mche unahitaji kinategemea mizizi yake imekwenda chini kiasi gani. Anza kumwagilia miche mara tu majani yake yanapoanza kusinyaa. Lakini ni vema kutosubiri mpaka hatua hii, kwani hudhoofisha mmea. Endelea kumwagilia kila mara unapoona udongo wa juu umekauka, hadi mche utakapootesha majani 2 au matatu.

Halafu, hadi utakapofikisha majani 5 au 6, mwagilia pale udongo utakuwa umekauka kiasi cha ukucha wa kidole gumba chako.

Tena hadi mizizi itakapoanza kutoboa kitako cha chombo, mwagilia pale utakapoona udongo umekauka kwenda chini kina cha nusu ya kidole gumba chako.

Palizi na kuweka mbolea

Magugu na miche ya miti hushindana kupata mwanga, maji na virutubisho vingine kutoka ardhini. Kiasi kidogo cha magugu kwenye chombo hakina madhara. Lakini yakizidi yaondoe kwa kuyakata kwa chini ili usibomoe udongo.

Iwapo ardhi yako ina rutuba, miche itapata virutubisho inavyohitaji. Kama mbolea inahitajika, tengeneza mbolea ya asili kutokana na samadi, mboji, au mkojo.

Kuhamisha miche kutoka kitaluni

EHB Ch11 Page 212-1.png
Umbali kati ya mche na mche
Umbali kati ya mche na mche
Umbali kati ya mche na mche
Upandaji katika umfumo wa pembe tatu husaidia miti mingi kuoteshwa katika eneo dogo.

Mizizi ya miche inapoanza kutoboa kitako cha chombo (kawaida miezi 3-4 baada ya kupanda), wakati wa kuihamishia mahali pake unakuwa umefika. Kama huwezi kuihamisha kipindi hiki, punguza urefu wa mizizi yake kwa kuikata kidogo mara moja kwa wiki. Hii husaidia mche kutengeneza shina la mizizi kama mviringo ndani ya chombo na siyo kujitokeza kuelekea ardhini.

Mwezi mmoja kabla ya kupanda, taratibu ondoa kivuli juu ya miche mpaka kufikia kiwango cha mwanga wa jua sawa na kule utakapohamishwa. Hii huifanya miche kuanza kuzoea hali ya jua na ukame wa sehemu itakapopandikizwa.

Siku moja kabla ya kupanda, mwagilia miche na kulowesha chombo. Ihamishe taratibu, ukichukua tahadhari kutoathiri mizizi. Weka alama kila mahali unapotaka kupandikiza mche. Umbali kati ya mti na mti hutegemea aina ya mti na sababu za kuipanda. Kwa ujumla, panda miti ili matawi yake yaweze kugusana tu pale itakapokua.

Ondoa magugu na mabaki ya miti iliyovunwa yote ambayo yanaweza kufunika miche au kushindana na miche kwa ajili ya maji ndani ya eneo la mita moja inayozunguka. Panda asubuhi mapema au jioni ili kukinga miti dhidi ya jua. Chukua tahadhari mizizi isiharibike au kukauka wakati wa kupanda.

EHB Ch11 Page 212-2.png
EHB Ch11 Page 212-3.png
Chimba mashimo ya pembe nne yenye kina cha mara moja na nusu ya vyombo vya miche. Mashimo ya mduara huzuia utanuzi wa mizizi hadi kwenye udongo unaozunguka. Jaza shimo na udongo ili shina la mche lilingane na usawa wa ardhi baada ya shimo kujazwa udongo. Unaweza kuongeza viganja viwili vya mboji au udongo mweusi wenye rutuba kusaidia mche kuanza kuota vizuri. Baada ya kupanda, lowesha udongo unaouzunguka mche na maji.

Kuhamisha miche kitaluni kwa ajili ya kupanda katika maeneo magumu

EHB Ch11 Page 213-1.png
Katika maeneo kame, tengeneza shimo dogo lenye mduara kwa ajili ya kudaka maji.
EHB Ch11 Page 213-2.png
Chimba mduara wa mita moja kwenye uelekeo wa juu ya mahali mti utakapopandwa na kutengeneza tungazi iliyo tambarare.
Jenga kizuizi kidogo kulinda tungazi isisombwe na maji.
Katika maeneo yenye mteremko mkali, tengeneza tungazi kwa ajili ya kila mti.
EHB Ch11 Page 213-3.png
Katika maeneo yenye mteremko wa kawaida, tengeneza tungazi za udongo zenye umbo la V uelekeo wa chini kutoka kwenye mti ili kudaka maji ya mvua.

Kutunza miti michanga

EHB Ch11 Page 213-4.png
Tengeneza uzio kulinda miti michanga.

Mti mchanga unahitaji kulindwa mwaka mzima wa maisha yake. Miradi mingi ya upandaji miti hushindwa kufanikiwa kwa sababu hakuna anayeisimamia miti michanga.

Iwapo hali ya hewa ni joto au ya ukame, miche inahitaji kumwagiliwa angalau mara moja kwa siku na baadaye kila baada ya siku 2 au 3. Baada ya wiki chache, mizizi ya miti huanza kutafuta maji yenyewe. Lakini kama hali ya joto inaendelea, mwagilia kadri miti inavyohitaji.

Dhibiti magugu mpaka mti utakapokuwa mrefu kuliko magugu hayo. Endapo wanyama au watoto wanaweza kuharibu miti hiyo michanga, jenga uzio kuzunguka mti.

Kama mti haukui vizuri, au majani yanaonekana kuwa ya njano au hayana afya, sambaza mbolea ya asili kuzunguka mti kadri ya matawi yake.



Ukurasa huu ulihuishwa: 04 Juni 2022