Hesperian Health Guides

Kuirudishia uhai wake ardhi iliyoharibiwa

Katika sura hii:

Wakati mwingine ardhi huharibiwa vibaya sana, kiasi cha kuonekana kwamba haiwezi kurejea tena hali yake ya kawaida. Katika maeneo ambapo ardhi yenye rutuba imegeuzwa kuwa jangwa, au mahali kemikali zenye sumu ardhini haziruhusu mimea kuota, ardhi inaweza kuchukuwa miaka mingi sana kurudia hali yake ya kawaida. Lakini katika maeneo mengi, juhudi zikifanyika kwa uangalifu na kukiwa na uelewa wa kutosha wa njia ambazo ardhi inavyoweza kurejea yenyewe katika hali yake ya kawaida, tunaweza kusaidia ardhi kurudisha uhai wake.

Hakuna mtu anayeweza kulazimisha ardhi iweze kuzalisha. Hata mbolea za viwandani hufanya kazi kwa muda mfupi na hatimaye ardhi huishiwa uwezo wa kuzalisha. Lakini kama tutazingatia mzunguko wa asili, tunaweza kuchangia kutengeneza mazingira ambayo ardhi inahitaji kurejea hali yenye afya na rutuba.

Ardhi yenyewe kurejesha uhai wake kwa njia za asili

Wakati mwingine njia bora ya kuifanya ardhi yenyewe kurejesha uhai wake ni kuiacha ipumzike, au kutumia njia mbalimbali kuisaidia kurejea hali yake ya asili. Kwa mfano, kuizungushia uzio, kuweka matangazo yanayokataza shughuli za watu katika eneo hilo, au kupunguza idadi ya mifugo ni miongoni mwa mbinu zinazoweza kusaidia ardhi kurejea hali yake tena.

A tall tree.

Ardhi inapolindwa na wakati huo huo hali ikawa inaruhusu, mimea inaweza kuanza kuota yenyewe. Ardhi yenyewe hurejesha uhai wake kwa njia za asili. Mchakato huu unaweza kuchukuwa miaka mingi au hata baada ya vizazi kadhaa kupita.

Ardhi yenyewe HAIWEZI kurejesha uhai wake iwapo:

  • Hakuna vyanzo vya mbegu au mimea asilia karibu.
  • Aina ya mimea inayoongezeka haraka imeshamiri na kufunika mimea inayohitajika.
  • Ardhi imeharibiwa na kuchafuliwa kiasi kwamba hakuna chochote ambacho kinaweza kuota.

Mimea na miti ya asili na isiyo ya asili

Mimea ya asili (mimea ya eneo fulani) huota kwa urahisi katika mazingira yake ya asilia. Pia hutunza bioanuwai kwa kuvutia na kutoa makazi kwa wadudu, ndege na wanyama.

Wakati mwingine mimea au miti ambayo si ya asili kwa eneo husika hugeuka kuwa maarufu kwa sababu huota na kukuwa haraka, hutoa mbao nzuri au huchangia kuboresha udongo. Miti kama vile mikaratusi, misonobari, miarobaini, na lusina imeoteshwa sehemu nyingi duniani. Hata hivyo, kupanda miti na mimea ambayo siyo asilia katika eneo lako kunaweza kuleta matatizo kwa eneo husika:

  • inaweza kufyonza maji mengi kutoka ardhini na kudhoofisha mimea na miti ya asili,
  • inaweza kusambaa haraka hadi mahali ambapo haitakiwi,
  • inaweza kusababisha wanyama na wadudu asilia katika eneo hilo kuhama na kutafuta makazi mengine.


Iwapo mimea ngeni itafunika eneo hilo, ni vigumu ardhi yenyewe kujirudishia uhai wake kwa njia za asili.

Mchakato wa ardhi yenyewe kujirejeshea uhai wake kwa njia asilia

Illustration of the below: Rain and sun on cracked, barren ground.
Illustration of the below: Rain and sun on ground with a few small plants.
1.   Ardhi iliyoharibiwa yenye udongo usio na rutuba na isiyo na mimea. 2.   Mimea midogo yenye ustamihilivu huchipua kwenye maeneo ambayo udongo unaweza kujikusanya. Mimea hii stamihilivu huhifadhi maji na kuvutia wadudu na ndege.
Illustration of the below: Rain and sun on small plants, birds and insects.
Illustration of the below: Plant roots growing down into soil.
Illustration of the below: Plants and a tree with deep roots.
3.    Maji hutuama kwenye vidaka maji vilivyotengenezwa na mimea stahimilivu, yakileta mbegu na virutubisho. Lakini ndege huleta mbegu zaidi. 4.   Mimea mikubwa zaidi na miti midogo huota. Mizizi yao hutenganisha ardhi ngumu na kutengeneza udongo laini ambao unaweza kuhifadhi maji. 5.   Mimea mikubwa zaidi na vichaka huota na kukua na hatimaye ardhi inakuwa imejirejeshea uhai wake


Jinsi ya kutengeneza mabonge ya mbegu

Njia rahisi ya kuotesha tena mimea katika eneo lililoathiriwa sana na mmomonyoko ni kutengeneza mabonge ya mbegu. Kila mwaka kusanya mbegu. Watoto hasa wana uwezo mkubwa wa kukusanya mbegu, na ni zoezi la kujifunza na burudani kwao. Kusanya mbegu nyingi kutoka miti asilia tofauti katika eneo lako, kadri iwezekanayo. Kwa kutumia mbegu hizi na udongo, tengeneza mabonge. Changanya: Mix:

EHB Ch11 Page 204-1.png
EHB Ch11 Page 204-2.png
EHB Ch11 Page 204-3.png
EHB Ch11 Page 204-4.png
Kipimo kimoja cha mbegu zilizochanganywa Vipimo viwili vya mboji au udongo laini Vipimo 3 vya udongo wa mfinyanzi uliochekechwa ili kuondoa mawe Kiasi kidogo cha maji

Changanya mbegu na mboji au udongo wa kupandia, kisha ongeza udongo wa mfinyanzi. Ongeza maji ambayo yanatosha tu kuulowesha. Ukiweka maji mengi mbegu zitajitokeza haraka. Viringa mabonge madogo kutokana na mchanganyiko huu na kuweka juani angalau kwa siku kadhaa.

EHB Ch11 Page 204-5.png


Siku chache kabla ya msimu wa mvua au wakati wa msimu wa mvua, nenda mahali unapotaka miti iote na kurusha mabonge hayo. Ni muhimu kuweka vizuizi mapema kuhakikisha mbegu hizo zisisombwe na maji ya mvua yanayotirika juu ya ardhi.


Mvua ikinyesha mbegu zitachipua. Mboji husaidi kutoa virutubisho, na udongo wa mfinyanzi huzuia mbegu zisikauke, zisiliwe na panya au ndege na zisipeperushwe. Baada ya mwaka mmoja mimea hiyo itatengeneza mbegu zake, na mimea mingi zaidi itaota. Udongo utajikusanya kwenye mimea na kudhibiti mmomonyoko. Baada ya muda aina nyingi ya mimea itaanza kuonekana. Iwapo hali hii haitavurugwa, baada ya miaka mingi, eneo zima litarejea asilia yake.


Kusaidia miti kujiotea yenyewe

A woman sitting beneath a dead tree.

Katika nchi ya Somalia, kuna miti michache kutokana na hali ya ukame inayokaribia jangwa. Idadi hiyo ya miti huzidi kupungua siku hadi siku kwa kuwa hukatwa kwa ajili ya kutengeneza mkaa. Sehemu ya mkaa hutumiwa ndani ya nchi lakini kiasi kikubwa huuzwa nchi za nje. Mwanamke mmoja wa Kisomali Fatima Jibrell alipoliona tatizo hili, alianza kampeni kuhamasisha watu kuacha kuuza mkaa nchi za nje. Aliuliza, “Sisi wenyewe hatuna miti ya kutosha, tutawezaje kuruhusu kunyonywa rasilimali hiyo kidogo iliyopo.?”


Kampeni yake ilifanikiwa kiasi. Lakini kwa wakati huo, ni miti michache ilikuwa imebaki. Hivyo alianza kampeni ya kupanda miti nchini Somalia. Aliamini kwa njia bora ya kuwapunguzia umasikini watu wake ni kurejesha tena miti Somalia.

Ardhi ya Somalia ni kavu na yenye joto kali, ni vigumu kustawisha miti. Pia kwa kuwa watu wa Somalia huhama hama kutoka sehemu moja hadi nyingine kutegemea na hali ya hewa, ni vigumu kupanda miti na kuitunza. Hivyo, Fatima akaanza kuwafundisha watu kutengeneza vizuizi vya kuta fupi za mawe kadri walivyokuwa wakihama. Japokuwa ardhi ni tambarare, Fatima aliamini kuwa maji yangetafuta mahali pa kutuama, yakiambatana na viumbe hai vingine. Wakati wa msimu mfupi wa mvua, kuta hizi zilisaidia kuzuia virutubisho vya udongo, na mimea na miti kuanza kujiotea yenyewe. Hivyo, kutokana na kampeni hiyo, idadi ya miti nchini Somalia iliongezeka kuliko awali. A tree beside a low rock fence.



Ukurasa huu ulihuishwa: 04 Juni 2022