Hesperian Health Guides
Maafa ya mlipuko wa gesi ya sumu ya Bhopal
HealthWiki > Mwongozo wa jamii juu ya afya ya mazingira > Sehemu ya tatu: Haki za kimazingira na upatikanaji wake > Maafa ya mlipuko wa gesi ya sumu ya Bhopal
Katika sura hii:
Mnamo usiku wa Desemba 3, 1984 katika jiji la Bhopal, India, maafa makubwa yalitokea. Kiwanda cha kutengeneza dawa za kuua wadudu ambacho kilikuwa katika eneo lenye watu wengi katika ukanda wanaoishi watu wenye kipato kidogo jijini Bhopal kilivujisha tani nyingi za gesi ya sumu kwenye hewa. Mfumo wa onyo ya tahadhari kiwandani ulizimwa, na jamii haikusikia kengele au kingora chochote kuashiria hatari.


Gesi ya sumu iliuwa watu wengi usiku huo. Baada ya siku 3 watu 8,000 walikuwa wamekufa. Lakini huu haukuwa mwisho wa maafa. Kwa ukweli huo ulikuwa ni mwanzo tu.
Baada ya miaka 20 iliyofuata, watu 20,000 walikuwa wamekufa kutokana na sumu iliyobaki kwenye miili yao. Wengi zaidi walikumbwa na matatizo makubwa ya kiafya yakiwemo maumivu na matatizo katika kupumua, kikohozi kisichopona, homa, ganzi mikononi na miguuni, udhaifu mwilini, uoga, msongo na saratani. Watoto na wajukuu wa walionusurika huzaliwa na matatizo makubwa ya viungo, yakiwemo miguu na mikono iliyodhoofu, kukua polepole,na matatizo mengi ya afya ya uzazi na mfumo wa neva. Zaidi ya watu 150,000 wameathirika kutokana na gesi ya sumu iliyovuja usiku huo jijini Bhopal.