Hesperian Health Guides

Jinsi mwanamke anavyopata mimba

Katika sura hii:

NWTND FP Page 4-1.png
Shahawa (manii): majimaji yenye mamilioni ya mbegu za kiume za uzazi, ambayo husafiri kupitia mrija huu na kutolewa nje kupitia uume
Uume
Makende: wanaume hutengeneza mbegu za kiume za uzazi kwenye makende yao
NWTND FP Page 4-2.png
Kinembe: sehemu yenye msisimko ambayo inaweza kutoa ashiki inapoguswa
Njia ya mkojo: mahali ambapo mkojo hutolewa nje
Njia/mlango wa uke
Mashavu ya uke
Njia ya kutolea kinyesi
Mifuko ya mayai ya kike (Ovari): baada ya wastani wa mwezi mmoja, mojawapo ya mifuko ya mwanamke ya mayai huachia yai la kike la uzazi lililopevuka kwenye njia au mirija ya kusafirisha mayai.
NWTND FP Page 4-3.png
Mrija wa kusafirisha mayai : yai la uzazi lilopevuka husafiri kwenye mrija huo na kuelekea kwenye mji wa mimba au tumbo la uzazi.
Mji wa mimba (tumbo la uzazi): mahali ambapo mtoto hukulia baada ya mwanamke kupata mimba.
Mlango wa mji wa mimba
Uke

Mwanaume anapofikia kilele na kuachia shahawa ndani au karibu na uke, shahawa kutoka kwenye ume huingia kwenye mji wa mimba au kizazi cha mwanamke na kwenye njia za kusafirisha mayai ya kike ya uzazi. Kama ni wakati wa kipindi cha rutuba(kipindi cha mwanamke kushika mimba), mbegu ya kiume inaweza kuungana na yai la kike lililopevuka. Kama mbegu ya kiume itarutubisha yai hilo, basi hujibanza kwenye ukuta wa mji wa mimba(kizazi). Hapo mimba itakuwa imetunga. Njia za uzazi wa mpango huzuia mimba kwa kuzuia mbegu za kiume kuingia kwenye uke, au kusimamisha mwili wa mwanamke usiachie mayai ya uzazi, au kuzuia mbegu za kiume kukutana na yai.