Hesperian Health Guides

Huduma ya ganzi

Maumivu tumboni, kuhara, na minyoo: Madawa

Lidokeini (Lidocaine), Lignokeini (Lignocaine)

Lidokeini (Lidocaine) ni dawa ya ganzi ambayo inaweza kuchomwa eneo linalozunguka kidonda kuachia ganzi ili mtu asisikie maumivu. Hii ni muhimu kabla ya kukamua jipu au kushona kidonda. Kama utaamua kuondoa damu iliyoganda kutoka kwenye bawasiri, tumia lidokeini kwanza.

Jinsi ya kutumiaNBgrninject.png

Choma sehemu mbili-ndani na chini ya ngozi inayozunguka eneo ambalo unakwenda kukata au kushona, ukiacha sentimeta 1 katikati. Kwanza, safisha ngozi vizuri, halafu choma sindano hiyo ya lidokeini. Tumia wastani mililita 1 ya dawa ya ganzi kwa kila sentimita 2 za ngozi. (Usitumie zaidi ya mililita 20 kwa pamoja.)

Angalia Dawa, vipimo, na matibabu (inaandaliwa) kuhusu jinsi ya kutoa huduma ya sindano kwa usalama.